• Karibu Hayate Organic Farms

    Kilimo Ndio Kauli Mbiu Yetu

  • Karibu Hayate Organic Farms

  • Karibu Hayate Organic Farms

    Karibu Hayate Organic Farms

About HAYATE ORGANIC FARMS

Hayate Organic Farms kampuni ya inayojishughulisha na kilimo cha mazao mbali mbali, kutoa huduma za usimamizi wa  mashamba,kusafisha mapori ya wateja  pamoja kuwapandia mazao wanayohitaji pamoja na kutoa huduma hizo pia tunatoa ushauri kwa watu wanaotarajia kuingia kwenye kilimo.

Mission

Hayate organic farms tunashughulika na kilimo cha matunda ya strawberry,blackberry na raspberry pamoja na miche yake kwa mkoa wa Mtwara tunalima zao la Korosho pamoja na miche yake pia tunauza korosho nyeupe za kula, kwa mkoa wa Tanga tunalima zao la Katani ( Mkonge) wilaya Handeni vijijini pamoja na kuuza miche yake bora pia kwa mkoa wa Pwani bagamoyo na Pangani tunalima zao la Nazi pamoja na kuzalisha miche yake bora kabisa mbegu aina ya Pangani one Hayate Organic Farms tunazalisha miche ya Karafuu,Hiriki,Mdarasini,miti ya mbao aina ya mitiki. Sambamba na hivyo tunatoa semina ya elimu kwa wakulima mbali mbali juu matumizi sahihi ya mbolea mashambani kwenye mazao yao, matumizi sahihi ya viwatilifu vyakuangamiza wadudu wahalibifu wa mazao,magonjwa ya mimea na jins yakuandaa shamba kwa ajili ya kilimo tunahakikisha tunawafikia kila kundi kila taasisi ya kidini shule mbali mbali elimu hii tunatoa bure ila kwa gharama za kuhudumia nauli,chakula na makazi kwa sehemu zinazohitaji huduma hizo kwa mkufunzi.

Vision

Hayate Organic Farms malengo ni kuhakikisha ifikapo 2025 tuwe tumeweza kuzalisha nazi kwa ukubwa wa Hekta 250 na kuanzisha kiwanda cha kukamua Mafuta ya Nazi kwa matumizi ya kula na kujipaka lkn pia sambasamba na hivyo tuna malengo yakutanua wigo mpana kwakuongeza mashamba makubwa kwa mkoa wa Tanga kwa ajili yakuzalisha zao la Katani ili tuwe msambazaji mkubwa ndani nje ya nchi. Lakini pia nikuhakikisha tunatoa ajira kwa wanawake na vijana ili kuhakikisha na wao wanajiongezea kipato na kuendesha Maisha yao na familia. Malengo yetu ifikapo 2025 tuwe tumeweza hamasisha vijana Zaidi ya 500 kujiajiri kwenye kilimo kwakuwapa elimu bure kwenye mashamba yetu huku wakipatiwa chakula na malazi bure kisha kujiunga kwa vikundi vya watu 5 kisha kuwaombea mkopo wa 10%  unaotengwa na halmashauri ya wilaya ambao hauna riba

Huduma Zetu

  • Kusafisha Mapori Kuwa Mashamba Safi Kwa Kilimo (Kufyeka Pori, Kung`Oa Visiki Na Kuingiza Trekta

  • Tunazalisha Miche Ya Nazi Mbegu Ya Pangani, Miche Ya Korosho Mbegu Ya Brazil Na Naliendele

  • Tunatoa Elimu Ya Kilimo Bure Kwa Mataasisi Kidini Na Mashuleni Pamoja Na Vikundi Vya Wanawake Na Vijana

  • Tunatoa Ushauri Kwa Watu Wanaotaka Kuingia Kwenye Kilimo Pamoja Na Kuwasimamia Kupata Mashamba Bora Kuyaanda Na Kulima Na Kusimamia

  • Tunatoa Huduma Za Kusimamia Miradi Ya Kilimo Kwa Wateja Wetu Wa Nje Ya Nchi Na Waajiriwa Ambao Muda Wao Ni Mchache Kusimamia Miradi Yao Ya Kilimo Waliyoianzisha (Farm Management & Supervision)

  • Tunatoa Huduma Kutembelea Mashamba Ya Watu Nakushauri Namna Yakufanya Kilimo Bora (Farms Visiting)

  • Tunatoa Huduma Ya Kupima Udongo Kwenye Mashamba Yaani (Soil Test) Kwa Mkoa Wowote Tunafika Na Kuupima Kwenye Maabara Ya Kisasa Na Tuna Waatalam Wa Udongo Waliobobea Kutoka Sokoine University Morogoro Na Nchini China

  • Tunatoa Huduma Ya Kuwaunganisha Wakulima Na Wateja Ili Kurahisha Masoko Ya Bidhaa Wanazo Zalisha Shambani Kwao Bila Malipo

Wasiliana Nasi